Zaburi 117 (NEN)

Zaburi 117
Sifa za Bwana
1 Msifuni Bwana, enyi mataifa yote;
mtukuzeni yeye, enyi watu wote.
2 Kwa kuwa upendo wake kwetu ni mkuu,
uaminifu wa Bwana unadumu milele.
Msifuni Bwana.117:2 Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.