Zaburi 122 (NEN)

Zaburi 122
Sifa kwa Yerusalemu
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.
1 Nilishangilia pamoja na wale walioniambia,
“Twende nyumbani mwa Bwana.”
2Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama
malangoni mwako.
3 Yerusalemu imejengwa vyema kama mji
ulioshikamana pamoja.
4 Huko ndiko makabila hukwea,
makabila ya Bwana,
kulisifu jina la Bwana kulingana na maagizo
waliopewa Israeli.
5Huko viti vya hukumu hukaa,
viti vya ufalme vya nyumba ya Daudi.
6 Omba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu:
“Wote wanaokupenda na wawe salama.
7 Amani na iwe ndani ya kuta zako,
na usalama ndani ya ngome zako.”
8Kwa ajili ya ndugu na rafiki zangu,
nitasema, “Amani iwe ndani yako.”
9 Kwa ajili ya nyumba ya Bwana Mungu wetu,
nitatafuta mafanikio yako.