Zaburi 131 (NEN)

Zaburi 131
Kumtegemea Mungu kwa unyenyekevu
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.
1 Moyo wangu hauna kiburi, Ee Bwana,
macho yangu hayajivuni;
sijishughulishi na mambo makuu kunizidi
wala mambo ya ajabu mno kwangu.
2 Lakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya
ndivyo ilivyo nafsi iliyo ndani yangu.
3 Ee Israeli, mtumaini Bwana
tangu sasa na hata milele.